Events

ZIC Yampongeza Ndugu Jape U. Khamis kwa Kuteuliwa Kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika

Zanzibar Insurance Corporation (ZIC) inampongeza kwa dhati Ndugu Jape U. Khamis kwa kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika. Uteuzi huu ni ishara ya imani na kutambuliwa kwa uwezo, uzoefu, na mchango wake katika kuimarisha utendaji wa taasisi.

ZIC inaamini kuwa chini ya uongozi wake, shirika litaendelea kuimarisha mifumo ya utawala bora, kuboresha utoaji wa huduma za bima, na kuongeza ufanisi wa kiutendaji kwa manufaa ya wateja, wadau, na maendeleo ya sekta ya bima kwa ujumla.

Shirika linamtakia kila la kheri katika kutekeleza majukumu yake mapya na linatoa ushirikiano kamili ili kuhakikisha malengo ya ZIC yanafikiwa kwa mafanikio.