Events

ZIC YASHIRIKI PUBLIC SERVICE INNOVATION AWARD 2026 – ZANZIBAR CLUSTER

Shirika la Bima Zanzibar (ZIC) limeshiriki katika hafla ya Public Service Innovation Award 2026 (Zanzibar Cluster) iliyofanyika katika Golden Tulip Airport Hotel. Hafla hii imelenga kutambua na kuthamini taasisi za umma zinazobuni na kutekeleza mifumo bora ya utoaji huduma kwa wananchi.

Katika tukio hilo, ZIC ilifanikiwa kushinda tuzo ya Public Service Innovation Award, ikiwa ni ushahidi wa juhudi zake katika kuimarisha ubunifu, ufanisi, na ubora wa huduma zinazotolewa kwa jamii. Ushindi huu unaonesha dhamira ya ZIC katika kuunga mkono mageuzi ya huduma za umma na kuchangia maendeleo endelevu ya Zanzibar.

ZIC itaendelea kuimarisha ubunifu na mifumo ya kisasa ili kuhakikisha huduma bora, za haraka na zenye kuaminika kwa wateja wake.