loader image

Uncategorized

Uncategorized

ZIC Sports Bonanza 2026 Promotes Health and Community Spirit in PembaNEW

The Zanzibar Insurance Corporation (ZIC) successfully hosted the ZIC Sports Bonanza 2026 at Gombani Grounds in the South Pemba Region, bringing together community members in a vibrant event focused on health, unity, and awareness.
The initiative aimed to encourage a culture of regular physical exercise while also educating the public on the importance of insurance in everyday life. The event was officially launched by the District Commissioner of Micheweni, Hon. Khatib Juma Mjaja, through a ceremonial walk that began at PBZ Chake Chake and concluded at the event venue.
In his address, Hon. Mjaja praised ZIC for its commitment to community development, highlighting the bonanza as a valuable platform for strengthening social bonds and promoting healthier lifestyles among citizens.
The one-day event featured a series of football matches involving multiple teams, creating an exciting and competitive atmosphere. The event was officially closed by the Permanent Secretary of the Ministry of Information, Youth, Culture and Sports, Mr. Mattar Zahor Masoud. Team Voxy emerged as the winner, earning qualification to represent Pemba in this yearโ€™s finals.
In his closing remarks, Mr. Mattar commended all participants for their enthusiasm and encouraged greater community participation in future editions. He also urged ZIC to continue organizing such impactful events annually.
Event Details:
๐Ÿ“… April 11, 2026
๐Ÿ“ Chake Chake, Pemba

Uncategorized

ZIC YAFUTARISHA WADAU WA BIMA ZANZIBAR KUIMARISHA USHIRIKIANO

Shirika la Bima la Zanzibar limeandaa hafla ya futari (Iftar) kwa wadau wake mbalimbali katika Hoteli ya Verde iliyopo Mtoni Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha mahusiano na ushirikiano kati ya shirika hilo na taasisi mbalimbali zinazoshirikiana nalo katika utoaji wa huduma za bima.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Mheshimiwa Dkt. Juma Malik Akil, ambaye alipongeza juhudi za Shirika la Bima la Zanzibar katika kuimarisha sekta ya bima
na kuchangia maendeleo ya uchumi wa Zanzibar kupitia huduma zake.
Katika hotuba yake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Bw. Ali Mzee Ali alieleza kuwa hafla hiyo ni sehemu ya utamaduni wa shirika wa kukutana na wadau wake katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, kujadiliana mafanikio yaliyopatikana pamoja na kuimarisha mikakati ya baadaye ya kukuza sekta ya bima Zanzibar.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Bima la Zanzibar, Bw. Jape Ussi Khamis, alisema shirika linaendelea kubuni na kuboresha huduma zake ili kukidhi mahitaji ya wananchi na taasisi mbalimbali, huku likiimarisha ushirikiano na sekta ya benki na wadau wengine muhimu.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na wakuu wa taasisi mbalimbali za umma na binafsi, madalali na mawakala wa bima, pamoja na wawakilishi wa mabenki yanayoshirikiana na Shirika la Bima la Zanzibar katika
utoaji wa huduma za bima.
Shirika la Bima la Zanzibar linaendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma za bima nchini na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya uchumi wa Zanzibar kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya fedha.

Uncategorized

ZIC TAWI LA DAR ES SALAAM LAANDAA IFTAR MAALUM KWA WAFANYAKAZI

Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) tawi la Dar es Salaam limeandaa hafla maalum ya Iftar iliyofanyika tarehe 4 Machi 2026 katika ukumbi wa Rotana jijini Dar es Salaam. Hafla hiyo iliandaliwa ikiwa ni sehemu ya kuendeleza mshikamano, ushirikiano na kuimarisha mahusiano miongoni mwa wafanyakazi wa shirika wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadan.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Ridhiwani Kikwete, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora). Katika hotuba yake, alilipongeza Shirika la Bima la Zanzibar kwa kuandaa hafla hiyo muhimu ambayo inaleta pamoja wafanyakazi katika mazingira ya kirafiki na ya kiimani. Alisisitiza umuhimu wa mshikamano, maadili mema kazini pamoja na kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuimarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi.
Aidha, alieleza kuwa matukio kama haya huchangia kujenga umoja na kuimarisha mahusiano kati ya wafanyakazi, jambo ambalo linaongeza ari ya kazi na kusaidia taasisi kufikia malengo yake kwa ufanisi zaidi.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na wafanyakazi mbalimbali wa Shirika la Bima la Zanzibar kutoka vitengo tofauti, ambapo walipata fursa ya kukutana, kubadilishana mawazo na kuimarisha ushirikiano wao. Vilevile, washiriki walipata muda wa pamoja wa kufutari na kuendelea kuzungumza kuhusu namna bora ya kuendeleza kazi za shirika na kutoa huduma bora zaidi kwa wateja.
Uongozi wa ZIC tawi la Dar es Salaam ulieleza kuwa shughuli hiyo ni sehemu ya juhudi za shirika katika kujenga utamaduni wa mshikamano na kuthamini mchango wa wafanyakazi wake. Pia ulisisitiza kuwa shirika litaendelea kuandaa shughuli kama hizo ambazo zinakuza mahusiano mazuri kazini na kuimarisha mazingira ya kazi.
Hafla hiyo ilimalizika kwa dua maalum na mazungumzo ya kirafiki miongoni mwa washiriki, hali iliyodhihirisha umoja na mshikamano uliopo ndani ya familia ya Shirika la Bima la Zanzibar.

Scroll to Top